Kero: karai kuwa beseni

Kero: karai kuwa beseni

***************************

 

kwetu ni injili ya kujichubua

kwa kwenda mbele ni kujikoboa,

 

ila, madhila hutufika, maji yazidipo unga,

ya ngozi kunadiwa, na gamba la nyoka

kuvulia utawala.

 

Eti tupinkele huleta njuru na mvua,

na sio kelele za kuamia kweleakwelea!

ndiposa ufisadi huu n’kaubatiza chuburexia.

 

Hata kama n’gombe mla nyasi

aweza kutoa kivazi cha harusi?

Je, ni iweje cha kutindikwa  

kwa jani la mchikichi,

kitoke na rangi ya chanikiwiti?

 

~ © Dr Morice, 2009.

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.